MAKONDA AMUAGIZA WAZIRI SILAA KUWACHULIA HATUA WATENDAJI WASIO WAAMINIFU.

KATIBU Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Paul Makonda akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam.
...........................

Timothy Marko

KATIBU Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Paul Makonda amemtaka Waziri wa Ardhi Nyumba na Makazi Jerry  Silaa kuwachukulia hatua Watendaji wa wizara hiyo waliobainika kudhurumu Haki za Wananchi katika  sekta ya Ardhi wachukuliwe Hatua za kisheria.

Akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam Paul Makonda amesema kuwa katika  sehemu nyingi katika ziara yake kumekuwa utendaji wa wadhuluma kwa baadhi ya watendaji wa Serikali husan katika sekta ya Ardhi.

"katika ziara nimebaini uwepo wa malalamiko mengi ya wananchi juu ya kuwepo na kukithiri kwa vitendo vya utoaji wa Hati feki na Nyaraka za za Ardhi" Alisema Katibu Mwenezi wa CCM Paul Makonda.

Makonda alisema Ni vyema Waziri wa Ardhi Nyumba na Makaazi Jerry Silaa kufanya Mapitio  utendaji sekta hiyo nakuwachukulia hatua za kisheria wanaodhulumu haki zawananchi.

Aliongeza kuwa kwa atayebainika mtendaji kudhurumu Mwananchi Ardhi wachukuliwe hatua za kisheria nawabainishwe.

"Ili kuondoa na kumaliza kabisa Migogoro ya Ardhi iliyokidhili nchini lazima Maeneo yote ya wazi yalindwe, Tumefikia hatua tuona mpaka watu  wanakatwa mapanga na wengine kuchomewa Nyumba zao kwa sababu ya Migogoro ya Ardhi" Alisisitiza Makonda.

katika hatua nyingine makonda amewataka viongozi wa serikali kutekeleza majukumu yao  kwa mujibu ya ilani ya Chama cha Mapinduzi 2020/25 hususani ibara ya 160 imezungumzia Utawala bora nakuwataka watendaji wote wa serikali wote nchini kuzingatia utawala bora.

0/Post a Comment/Comments