
Kamishna
Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Aretas Lyimo akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es salaam akitoa tathimini kuhusu operesheni waliyoifanya
kwa ushirikiano na Vyombo vingine vya Ulinzi na usalama na TFS katika mikoa ya Shinyanga,Tabora,Iringa,Mbeya,Arusha
na Dar es salaam.
Baadhi
ya Dawa za kulevya zilizokamatwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa
za Kulevya katika operesheni waliyoifanya kwa ushirikiano na Vyombo vingine vya
Ulinzi na usalama na TFS katika mikoa ya Shinyanga,Tabora,Iringa,Mbeya,Arusha
na Dar es salaam.Madawa
ya kulevya yakiteketezwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya
NA
MUSSA KHALID
Mamlaka
ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imefanikiwa kukamata Jumla
ya Kilogram 54,506.553 za dawa za kulevya
mashambani na viwandani pamoja na kuteketeza ekari 262 za mashamba ya
bangi katika mikoa mbalimbali nchini.
Hayo
yamebainishwa leo jijini Dar es salaam na Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya
Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Aretas Lyimo wakati akitoa tathimini
kuhusu operesheni waliyoifanya kwa ushirikiano na Vyombo vingine vya Ulinzi na
usalama na TFS katika mikoa ya Shinyanga,Tabora,Iringa,Mbeya,Arusha na Dar es
salaam.
Kamishna
Lyimo amezitaja Dawa zilizokamatwa kuwa ni bangi Kilo 54,589.65,mirungi Kilo
10.3,Heroin gramu 90.93,Cocain gramu 1.98 na Kilogram 4.623 za aina mpya ya
Dawa za kulevya Methylene dioxy Pyrovalerone (MDPV) iliyokamatwa jijini Dar es
salaam ikisafirishwa na raia wa Comoro aitwaye
Ahmed Bakar Abdou (32).
Aidha
amesema kuwa watuhumiwa 72 wamekamatwa kuhusika na dawa hizo na baadhi yao
tayari wamefikishwa mahakamani.
Kuhusu
Dawa ya MDPV,Kamishna Lyimo amesema ni mpya ya kulevya iliyo katika kundi la
vichangamshi inayotengenezwa kwa kutumia kemikali bashirifu na husababisha
madhara ya haraka kwa mtumiaji ikilinganishwa na nyingine.
‘Dawa
hii ya kulevya huuzwa kwa njia ya mtandao na husafirishwa kupitia kampuni za
usafirishaji vifurushi na hufichwa kwa kuwekwa chapa za majina bandia kama bath
salts,Ivory Wave,Plant Fertilizer,Vanilla Sky na Energy’amesema Kamishna Lyimo
Katika
Hatua nyingine Mamlaka hiyo imebaini uwepo wa mashamba makubwa ya bangi katika
hifadhi za misitu Ubangu mkoani Shinyanga na mabatini Mkoani Tabora ambapo
wahalifu hao wamekata miti katikati ya misitu hiyo na kulima bangi.
Hata hivyo Kamishna huyo wameendelea kuwasisitiza wananchi kuonyesha ushirikianao kwa kutoa taarifa sahihi za wazalishaji na wauzaji wa dawa za kulevya katika maeneo yao ili kuweza kufanikisha operesheni mbalimbali wanazozifanya.
Post a Comment