DART KUANZA MFUMO WA KADI JANJA, KUACHANA NA KARATASI

 


       *************

Na Magrethy Katengu Dar es salaam

Wakala wa Mabasi yaendayo haraka (DART) leo wamefunga mafunzo kutoka kwa wataalamu wa idara ya Tehama  ambayo yamejikita katika kadi janja zitakatumika katika  mfumo wa nauli kabla ya abiria  kuiingia kwenye geti anatumia kadi badala ya kulipa nauli keshi.

Akizungumza  leo Mei 17,2024 Mkurugenzi wa Wakala wa Mabasi yaendayo haraka Dart,  Athumani Kihamia wakati wa kufunga mafunzo hayo ya siku 5 kwa wahitimu 10 yaliolenga utunzaji wa usalama za kadi janja na nywila zake kutoka kampuni ya Adva ID kutoka nchini India.

Hata hivyo Mkurugenzi amefafanua kuwa, hadi sasa mageti zaidi ya 300  yaliyogharibu zaidi ya bilion 11 na ujenzi wake umeshaanza na kufikia 67% itasidia kudhibiti mapato kwa watumishi wasio waaminifu,.

"Kadi janja ni kadi zinazotumika katika mfumo wa nauli lengo la Dart ni kufunga  maeneo mengi huku  timu kubwa ya vijana mahiri ambao tutakaa nao kwa miaka 10 ili iwe rahisi kupeana ujuzi na vijana wengine wapya watakao ajiriwa, tunataka kuboresha mifumo yetu ili tutoe huduma zenye ubora"amesema Kihamia.

Hata hivyo, amesema kuwa siku chache zijazo baada ya mwezi wa 6 wataanza kutumia mageti hayo ambapo wameshaingiza mageti janja kutoka nje zaidi ya 300, yatatumika katika mfumo wa nauli yataepusha katika uvujaji wa nauli, mapato na watumishi wasio waaminifu, pamoja na kuokoa muda.

Naye Mkurugenzi wa teknolojia habari na mawasiliano Dart Ng'wanashigi Gagaga amesema baada ya Mafunzo ya  kujenga uwezo wa timu ya    wanaoshughulikia mfumo wa nauli katika mageti yatakayotumia na  kadi na   mpaka sasa kituo cha Korogwe kimeshakamilika na vingine vinaendele na matengenezo.

"Ubora wa Mageti haya janja yatakayofungwa mfumo maalumu  na kuanza kutumika abiria atakapofika na kadi yake itamwonyesha kiasi cha fedha kama hakitoshelezi akaongeze hivyo hakutakiwa na matumizi yeyote ya karatasi tuko kidigital zaidi " amesema Mkurugenzi Tehama .

Naye Muhitimu wa Mafunzo hayo Jackson Kazaura ameshukuru kupata mafunzo hayo hivyo ameahidi ujuzi huo anakwenda kuutumia na kufundisha wengine .

Naye Mwakilishi wa Wataalamu Kampuni waliyotoa mafunzo  Kadi janja Advan IDe, Duncan Chege amesema wanaamini mafunzo hayo waliyotoa wakufunzi  wataenda kutekeleza progaram hiyo kwa weledi zaidi huku wakiwafundisha na wengine ambao hawakupata fursa ya kuhudhuria .

Awali mafunzo hayo yaliwahi kutolewa mwaka 2000 lakini kutokana na kuhamishwa hamishwa wakurugenzi hivyo yametolewa mwaka huu 2024 na wataalamu hawa wataanza kuyafanyia kazi.

Aidha onyo kali limetolewa kwa  madereva wanaoendesha magari ya serikali na maboda boda na magari binafsi kuacha mara moja  kutumia njia ya mwendokasi bila kibali maalum kwani kufanya hivyo ni kuvunja sheria na kusababisha ajali zisizo za lazima.




0/Post a Comment/Comments