NA Mwandishi wetu
Imeelezwa kuwa akili
mnemba (IA), itasaidia kuongeza tija na ushindani wa Biashara huku elimu zaidi
ikihitajika kwa wadau na wananchi kuhusu Teknolojia hiyo.
Kauli hiyo imetolewa Jijini Dar es Salaam, na Mkurugenzi Mkuu wa
Tume ya Ushindani (FCC), William Erio, katika kongamano la siku moja la
kujadili matumizi ya akili mnemba yanayozingatia haki na uwajibikaji kwa mlaji.
Erio amesema kuwa hivi sasa
Biashara nyingi zinafanywa kwa njia ya mifumo ya kimtandao na huduma nyingi
zinatolewa na akili mnemba, hivyo FCC inaangalia jinsi ambavyo inaweza kutumia
Teknolojia hiyo kumlinda mlaji kwa mujibu wa kanuni na Sheria
Kwa upande wake
Mwenyekiti wa Bodi ya FCC, Dk Agrey Mlimuka amesema kuwa azma hiyo itakuwa na
maana pale mifumo ya kiteknolojia itazingatia uwajibikaji ,tija, ,haki na usawa
kwa kuwekewa mifumo thabiti ya usimamizi na udhibiti.
Naye Mwenyekiti wa Baraza
la Ushindani, Jaji Salma Maghimbi amasema lazima wawe sehemu muhimu kwa
kuangalia teknolojia hiyo ili kumlinda mlaji kutokana na uwezo wake mkubwa wa
kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja.
kongamano hilo
limejumuisha wadau na watalaam mbalimbali wakiwemo TEHEMA, Vyuo Vikuu, Taasisi
za Utafiti , Afya, Sera na Sheria, pamoja na wafanyabiashara kutoka Sekta
Binafsi.





Post a Comment