KIMBUNGA "IALY" CHAFIKA MWISHO

............

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema kuwa mwenendo wa mifumo ya hali ya hewa unaonesha kuwa katika kipindi cha saa 6 zilizopita, Kimbunga “IALY” kimepoteza kabisa nguvu yake, kikiwa kaskazini mashariki mwa pwani ya Kenya.

 Kwa mujibu wa Taarifa ambayo imetolewa na Mmlaka hiyo imesema kuwa  kwa sasa hakuna tena tishio la kimbunga “IALY” katika nchi yetu. 

Aidha, imesema kuwa wakati kikipita karibu na pwani na nchi yetu kati ya  tarehe 21 na tarehe 22 Mei 2024 kimeweza kusababisha vipindi vya mvua, upepo mkali na mawimbi makubwa katika maeneo ya pwani ya nchi yetu kama ilivyotabiriwa awali.

Hata hivyo ikumbukwe kuwa, japo tunaelekea mwishoni mwa msimu wa Masika, 2024,inakaribia kuanza kwa msimu wa Kipupwe, na kwasababu hiyo, vipindi vya upepo wa Kusi baharini vinaweza kuanza kujitokeza na kuambatana na mawimbi makubwa kwa baadhi ya nyakati.

Wananchi na watumiaji wa bahari wanashauriwa kuendelea kufuatilia na kuzingatia taarifa za utabiri kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania pamoja na maelekezo na miongozo inayotolewa na mamlaka husika.Imetolewa na: Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania.

0/Post a Comment/Comments