MAENDELEO BENKI YATOA BIL 9.8 KWA WAMACHINGA.

Mkurugenzi Mtendaji wa Maendeleo Bank, Dkt. Ibrahim Mwangalaba Kushoto na Mwenyekiti wa Machinga Dar es Salaam, Namoto Yusuf Namoto wakibadilishana Mkataba mara baada ya kusaini Mkataba wa Makubaliano ya Mradi wa kwanza wa Ununuzi wa Viwanjaa vya Wamachinga wa Kariakoo jinini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Maendeleo Bank, Dkt. Ibrahim Mwangalaba Kushoto aliyekaa Mwenyekiti wa Machinga Dar es Salaam,Namoto Yusuf Namoto wakisainiMkataba wa Makubaliano ya Mradi wa kwanza wa Ununuzi wa Viwanjaa vya Wamachinga wa Kariakoo jinini Dar es Salaam leo mei 07 2024. Wa Mwisho waliyekaa ni Mmiliki wa Ardhi iliyopo kijiji cha Magoza Mkuranga, Kondo Maulid Mkangala.

Mkurugenzi Mtendaji wa Maendeleo Bank, Dkt. Ibrahim Mwangalaba Kushoto na Mwenyekiti wa Machinga Dar es Salaam, Namoto Yusuf Namoto wakionesha mikataba mara baada ya kusaini Mkataba wa Makubaliano ya Mradi wa kwanza wa Ununuzi wa Viwanjaa vya Wamachinga wa Kariakoo jinini Dar es Salaam leo Mei 07, 2024.
Mwenyekiti wa Machinga Dar es Salaam, Namoto Yusuf Namoto akizungumza na waandishi wa habari wakatiwa kusaini Mkataba wa Makubaliano ya Mradi wa kwanza wa Ununuzi wa Viwanjaa vya Wamachinga wa Kariakoo jinini Dar es Salaam leo Mei 07,2024. Katikati ni Mkurugenzi Mtendaji wa Maendeleo Bank, Dkt. Ibrahim Mwangalaba.

                                             

                                                      *******

Na.Timothy Marko

MAENDELEO Benki imetoa mikopo ya Shilingi Bilioni 9.8 katika kuwawezesha Wafanyabiashara wadogowadogo wapatao700 wa jiji la Dar es salaam itakayo wawezesha kupata Maakaazi  ya Nyumba  500.

Akizungumza waandishi wa Habar jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Maendeleo Benki Ibrahim Mwangalaba, amesema mpango huo utawezesha wamachinga kumiliki ardhi na Makazi  bora ili kuliwezesha kundi hilo kukopesheka kwenye Mabenki.

" Kwa mpango huu utawawezesha kukidhi vigezo vya kukopesheka ili kukuza mitaji  kwa sababu watakuwa wanakidhi Sharti la Uwepo wa dhamana ya mikopo ambayo ndio limekuwa kikwazo kikubwa cha kukopesheka kwa wamachinga walio wengi"Alisema Mkurugenzi Ibrahimu Mwangalaba.

Mwangalaba aliongeza kuwaDhamira ya Benki hiyo nikuwainua Wamachinga na wafanyabiashara wadogowawogo kutoka kwenye nafasi hiyo kwenda kuwa wafanyabishara wakubwa.

Alisisitza kuwa Hatua hiyo itawezesha ukuaji wa Uchumi na Uzaliishaji na ulipaji wakodi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wamachinga wa Mkoa wa Dar es Salaam, Namoto Yussufu Namoto, amesema kuwa wafanyabiashara hao wametengeneza kanzi data ya wafanyabiashara wa mkoa huo ambapo zaidi masoko17 yanatambulika najumuya hiyo.

Alisema Hadi kufika Mwezi huu zaidi ya shilingi bilionj19.2 zimeweza kukopeshwa kwa wafanyabishara hao.

"Wamachinga 700 wamekopeshwa viwanja milioni 500 vyenye thamani ya shilingi bilioni 10"Alisema Mwenyekiti wa wamachinga mkoa wa Dar es salaam Namoto  yusufu


0/Post a Comment/Comments