Shule ya Mbezi na Ufundi Manispaa ya Ubungo
************
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
MKUU wa Shule ya Msingi Mbezi na Ufundi , Manispaa ya
Ubungo, Kata ya Mbezi , Ndugu Daniel Machage amesema kwamba michango yote kwa
ajili ya mitihani ya mihura na Moko inafanywa baada ya kikao cha wazazi
kuridhia kama muongozo wa wizara ya elimu na ufundi unavyotaka kwa kuwa Shule
za serikali ni mkombozi wa elimu hapa
nchini.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake leo
asubuhi jijini Dar es Salaam, Bw Machage amesema kwamba kila mwezi wa Juni huwa
wanafanya kikao na wazazi shule hapo ili kupata maendeleo ya kitaaluma kwa
maslahi mapana ya Watoto wa kitanzania.
“sio kweli kwamba mimi nakusanya michango kwa wanafunzi
kupitia wazazi wao bila kufanya nao vikao Hapana huwa tunakuwa na vikao hapa
tena safari hii nataka mje kwenye kikao , na naweka na (speakers) kubwa mpaka
kule stendi ya magufuli wanasikia hii yote ni kwa manufaa ya hawa wananchi na
Watoto wa hapa mbezi,”amesema kwa
msisitizo
Aliongeza kwamba ni kweli fedha kutoka serikali zinakuja
kupitia Tamisemi kiasi cha shilingi 1.2 milioni kila mwezi ila ni kwa ajili ya
ukarabati wa shule , miundombinu , vifaa na mambo ya michezo Pamoja na gharama
zingine ila haitoshi kwa kweli lakini siwezi kukusanya fedha bila idhini ya
wazazi , Mkurugenzi na kibali cha Mkuu wa Wilaya (DC)
“Katika hiyo fedha 1.2 millioni utoe 2% ili uweze kugharamia
mitihani ya mihura, moko nay a kata kwa wanafunzi wasipoungua 2,532 na darasa
la saba pekee ni wanafunzi 291 hii (capitation) ya serikali haiwezi kutosha
ndugu zangu,”alisisitiza kwa sauti ya upole
Aliendelea kusema kwamba Mkuu wa Wilaya ya Ubungo ingawa hakutoa maandishi ila yatakuja amesema
kwamba kwa madarasa ya mitihani kila wiki wanaweza kuchangia 1500 na kwa
madarasa ambayo hayana mitihani kila mwezi 1000.
“Sasa sie hapa tunajibana bana kwa fedha ya madarasa ambao
hawana mitihani tunakusanya kila mwezi tunagharamia mitihani ya kata hapa shule
ya mbezi mitihani ya kata hatukusanyi michango kutoka kwa wazazi,’ alisema kwa
kujiamini .
Aliendelea kusema kwamba shule za serikali ni mkombozi kwa
watanzania wengi hapa nchini kwa sababu watu wanapata nafasi ya kusomesha
Watoto wao kwa gharama ndogo na wanapata elimu nzuri.
Awali mwandishi wa habari hii alimtafuta mwalimu huyo mkuu
kutoa ufafanuzi wa tuhuma mbalimbali ikiwemo ya kukusanya michango kwa
wanafunzi, kutumia lugha zisizo na staha kwa walimu na mahusiano mabaya na
wenzake.
Akifafanua juu ya tuhuma hizo alisema kwamba sio kweli
kwamba yeye anatumia lugha za mbaya ni kusimamia kanuni, sheria na taratibu za
serikali katika kuhakikisha taaluma inapanda shule hapo.
“kama mimi ningekuwa na mahusiano mabaya na walimu wangu
nisingeweza kupandisha kiwango cha ufaulu cha shule hii kwa sababu ufaulu
unapanda kwa sasa shule hii ni ya 20 katia 80 katika wilaya ya Ubungo
tunakwenda vizuri kwa kweli.
Kwa Upande wake, Afisa Elimu wa Wilaya ya Ubungo, Ndugu
Denis Nyoni alisema kwamba michango yote inayokusanya shule lazima kuwa na
vikao kati ya wazazi na uongozi wa shule na wazazi wanarishia kuchangia gharama
za elimu hapa nchini.
“sikia ndugu yangu fedha za serikali zinakwenda kila mwezi
ila pale ambapo hapakutosha wanaweza kukusanya michango kama waraka wa serikali
unanyosema na kibali kinatoka kwa Mkuu wa Wilaya (DC) na si vinginevyo,”alisisitiza
Ndugu Nyoni
Ndugu Nyoni aliongeza kwamba taratibu zote za serikali
zinafuatwa na sio kweli kwamba Mwalimu Mkuu wa hapo mbezi anafanya kwa matakwa
yake mengine watu wanakuwa na maslahi yao kwa kweli (interest zao) ila kama
kuna tofauti naweza kufuatilia.
Kwa Upande Mratibu wa Elimu Kata ya Mbezi, Bi Suzana Massawe
amesema kwamba upande hajawahi kupata malalamiko hayo ya ukusanyaji wa michango
ua mitihani shuleni hapo kama yapo anafuatilia.
Awali kulikuwa na
tuhuma dhidi ya Mkuu huyo wa Shule ya Mbezi kwa anafanya unyanyasaji kwa walimu
, kukusanya michango bila vikao na wazazi na kuendesha shule kinyume na matakwa
ya serikali.
Taarifa za awali zilidai kwamba Mwalimu Mkuu huyo nim babe ,
ana kiburi , anatoa lugha zisizo na staha kwa walimu wa kike na kufanya matendo
ambayo ni kinyume cha maadili kwa viongozi wa umma.
Mwisho .


Post a Comment