************
Na Mwandishi Wetu
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imesema kuna uwezekano wa kutokea kwa Kimbunga kamili hadi kufikia
kesho tarehe 2 Mei 2024 kutokana
na uwepo wa mgandamizo mdogo wa
hewa katika Bahari ya Hindi mashariki mwa pwani ya Mtwara.
Kupitia taarifa iliyotolewa
na mamlaka hiyo leo Mei 1, 2024 imesema Wakati mgandamizo huo mdogo wa hewa
ukiendelea kuimarika, unatarajiwa pia kusogea kuelekea baadhi ya maeneo ya pwani ya nchi kuanzia
usiku wa kuamkia siku ya Ijumaa
tarehe 3 Mei 2024.
Aidha taarifa hiyo imedai Mgandamizo
huo mdogo wa hewa unatarajiwa kuendelea kuwepo
katika maeneo ya ukanda wa pwani ya nchi hadi tarehe 6 Mei 2024.
Hata hivyo,mgandamizo huo mdogo wa hewa
unatarajiwa kupungua nguvu baada ya tarehe 6 Mei 2024.
TMA imewataka Wananchi kuendelea kufuatilia na
kuzingatia taarifa za utabiri
kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania pamoja na
kupata ushauri na miongozo ya
wataalam katika sekta husika ili kujikinga na
athari zinazoweza kujitokeza.
Uwepo wa mgandamizo huo
mdogo wa hewa unatarajiwa kutawala na kuathiri mifumo ya hali ya hewa hapa nchini ikiwa ni pamoja na kusababisha
vipindi vya mvua kubwa na upepo mkali katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Mtwara, Lindi,
Pwani, Morogoro, Dar es Salaam na maeneo ya jirani.

Post a Comment