Na Lilian Ekonga
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kongamano hilo linalotarajiwa kufanyika Jumatatu Mei 20, 2024 katika ukumbi wa maktaba katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
Akizungumza na waandishi wa habari leo Mei 18, 2024 Jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa JUMIKITA Shaaban Matwebe amesema Kongamano hilo linatarajiwa kuwa na washiriki zaidi ya 500, ambapo mada mbalimbali zitajadiliwa ikiwa ni pamoja na mitandao ya kijamii na uzalendo, fursa zilizopo kwenye tasnia hiyo, mafanikio na changamoto ili kutoa mchango wa kiundeshaji kwa wadau kupitia JUMIKITA.
"Tutatoa pia mapendekezo yatakayosaidia serikali kwenye uratibu wa sera za jinsi ya kuunganisha sayansi ya uchumi wa taarifa (information economics) na uchumi wa taarifa (information economy)". Amesema
Aidha amesema kuwa Kongamano hilo litajadili mafanikio ya miaka mitatu ya serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan ikiwa ni pamoja na maadhimisho ya siku ya uhuru wa habari duniani.

Post a Comment