MWENYEKITI CCK AHAMASISHA USHIRIKI DAFTARI IA KUDUMU IA WAPIGA KURA MUDA UTAKAPO FIKA

Mwenyekiti wa Chama cha Kijamii (CCK) Taifa David Daud Mwaijojele akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake Magomeni jijini Dar es salaam..

...................

NA MUSSA KHALID

Mwenyekiti wa Chama cha Kijamii (CCK) Taifa David Daud Mwaijojele amewahamasisha Watanzania kutumia fursa ya kujitokeza kwa wingi kushiriki kujiandikisha kwenye Daftari Ia Kudumu Ia Wapiga Kura muda utakapo fika ili waweze kwenda kumchagua kiongozi aliyebora wakati wa uchaguzi.

Mwaijojele amesema hayo jijini Dar es salaam wakati akizungumza na kituo hiki akieleza msimamo wa chama chao katika kuhamasisha wanachama kushiriki katika zoezi hilo ambalo hivi karibu Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imetangaza kusogezwa mbele kwa zoezi Ia uboreshaji wa Daftari Ia Kudumu Ia Wapiga Kura hadi tarehe 20 Julai, 2024 badala ya tarehe 01 Julai, 2024 iliyopangwa hapo awali.

Mwenyekiti huyo amesema kuwa kujitokeza kwao kwa wingi itawasaidia kurekebisha taarifa zao kwa usahihi kwani malengo yote yanayowekwa ni kwaajili ya kulijenga taifa la Tanzania.

Awali akizungumzia kuhusu mipango ya chama cha CCK ni kuhakikisha watanzania kwanza wanaishi kwa uzalendo ikiwemo kuwaletea wananchi maendeleo katika maeneo yao.

‘Sisi CCK tunahitaji mifumo mizuri ya kuwaletea wananchi maendeleo na vyakula hivyo lengo letu pia ni kuhakikisha mtanzania anafurahia maisha na uchumi anafanya kilimo chenye tija cha kuwalete maendeleo’amesema Mwaijolele

Aidha Mwenyekiti huyo amesema kuwa kuwepo na utulivu nchini ndio utasababisha kuleta maendeleo hivyo amewataka wanasiasa kukubaliana na matokeo zitakapofika nyakati za uchaguzi.

Amesema CCK ndio chama pekee kitakachowawezesha wananchi kuwa na maendeleo katika maeneo hivyo amewataka muda utakapofika wahakikishe wanachagua watu sahihi kwa muda sahihi kutoka chama cha kijamii.

Akizungumzia wanasiasa ambao wameahidi maendeleo na hawakutekeleza katika mitaa,Kata au Majimbo yao,ni vyema wananchi wakafanya maamuzi sahihi kwa kufanya mabadiliko katika nafasi hizo.

Katika Hatua nyingine Mwaijolele ameipongeza serikali kwa kufanya mambo mazuri kwa ajili ya kuibadilisha nchi hii huku akisema kuwa licha ya hayo yote haitajiki kiongozi mzembe katia utendaji wake wa kazi.

Amewataka watanzania zinapofika nyakati za uchaguzi wabadilike kwa kuepuka kupokea zawadi kutoka kwa wanasiasa badala yake wahakikishe wanachagua watu sahihi kwa ajili ya maendeleo ya Taifa.

0/Post a Comment/Comments