NCC YAWAJENGEA UWEZO WADAU WA SEKTA YA UJENZI

Mkadiriaji Majenzi kutoka Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) Elias Kissamo wakati akizungumza kwenye mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo wadau wa sekta ya ujenzi kuhusu namna ya  kusuluhisha migogoro inayohusu sekta hiyo ambayo yameratibiwa na Baraza hilo ambayo yanafanyikia jijini Dar es salaam.Jaji Mstaafu wa Mahakama kuu ya Tanzania Dkt Fauz Twaib akitoa mafunzo maalum kwa ajili ya kuwajengea uwezo wadau wa sekta ya ujenzi kuhusu namna ya  kusuluhisha migogoro inayohusu sekta hiyo ambayo yameratibiwa na Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) ambayo yanafanyikia jijini Dar es salaam.Mkadiriaji Majenzi kutoka Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) Anitha Mallewo akifuatilia kwa makini mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo wadau wa sekta ya ujenzi kuhusu namna ya  kusuluhisha migogoro inayohusu sekta hiyo ambayo yameratibiwa na Baraza hilo ambayo yanafanyikia jijini Dar es salaam.Baadhi ya wadau ambao wameshiriki kwenye mafunzo maalum ya kujengewa uwezo kuhusu namna ya  kusuluhisha migogoro inayohusu sekta Ujenzi ambayo yameratibiwa na Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) ambayo yanafanyikia jijini Dar es salaam.

Picha ya pamoja akiwemo Jaji Mstaafu wa Mahakama kuu ya Tanzania Dkt Fauz Twaib, Mkadiriaji Majenzi kutoka Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) Elias Kissamo, Mkadiriaji Majenzi kutoka Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) Anitha Mallewo na wadau mbalimbali katika mnyoro wa sekta ya ujenzi na sheria ambao wameshiriki kwenye mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo wadau wa sekta ya ujenzi kuhusu namna ya  kusuluhisha migogoro inayohusu sekta hiyo ambayo yameratibiwa na Baraza hilo ambayo yanafanyikia jijini Dar es salaam.
......................

Imeelezwa kuwa Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia Suluh Hassan imekuwa na mchango mkubwa katika kuhakikisha usuluhishi wa migogoro katika sekta ya ujenzi unafanyika kwa kufata taratibu zinazoheshimika ndani na nje ya nchi.

Hayo yameelezwa leo jijini Dar es salaam na Mkadiriaji Majenzi kutoka Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) Elias Kissamo wakati akizungumza kwenye mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo wadau wa sekta ya ujenzi kuhusu namna ya  kusuluhisha migogoro inayohusu sekta hiyo ambayo yameratibiwa na Baraza hilo.

Kissamo amesema kuwa mafunzo hayo yatawasaidia washiriki kuwa na elimu ya kufahamu namna ya kufanya utatuzi wa migogoro katika sekta ya ujenzi nje ya mahakama.

Aidha Kissamo amesema Baraza la Taifa la Ujenzi limeundwa kwa ajili kuangalia maendeleo ya ujenzi nchini ikiwemo kuwa na njia sahihi za kusimamia katika usuluhishi migogoro.

‘Baraza linasimamia usuluhisi na sio msuluhishi kwani linachagua wasuluhishi ambao wapo kwenye mpangilio wanaosaidia katika kusuluhisha’amesema Kissamo

Awali akizungumza Jaji Mstaafu wa Mahakama kuu ya Tanzania Dkt Fauz Twaib amesema kutokana na kuwepo kwa migogoro imeonekana kuwe na haja ya kuwa na mfumo mbadala mbali na wakimahakama kwa ajili ya kutatua migogoro.

‘Kuna mambo mengi ambayo unaweza kuyaepuka kwa kutumia mfumo mbadala mmoja wapo ni kujaribu kupunguza muda ambao utatumika kutatua migogoro kwani unapokwenda mahakani utachukua muda mrefu zaidi kwani kuna mfumo wa kukata rufaa ambayo inapoteza muda lakini pili mahaka ina utaratibu lazima uufate ili uweze kutatu migogoro’amesema Dkt Twaib

Dkt Twaib amesema kuwa wale ambao wanafanya kazi za Abitration mara nyingi wana ujuzi na uzoefu katika hiyo fani ikiwemo katika matumizi ya nyenzo katika ujenzi na gharama zake.

Kwa upande wake Mshiriki wa mafunzo hayo rehema Mtulya ambaye ni Wakili wa serikali kutoka Ofisi ya Wakili Mkuu wa serikali amesema mafunzo hayo yatamsaidia katika uendeshaji wa mashauri ya usuluhishi katika kazi zake za kila siku.

Pia ametumia fursa hiyo kutoa ushauri kwa wadau mbalimbali kuhudhuria mafunzo hayo kwani yataweza kuwasaidia katika kuepukana na migogoro kwani kwani katika mikataba mbalimbali inawagusa wananchi.

0/Post a Comment/Comments