SAHARA SPARKS KUTIKASA MWAKA HUU,MTAMBALIKE AGUSIA MITAJI KWA WABUNIFU.


 ***********

KUKOSEKANA kwa mitaji ,tatizo la sera ni changamoto ambayo inawakumba wabunifu kufikia malengo yao.

 Hayo yamebainishwa leo mapema jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Sahara adventures,Jummanne Mtambalike wakati akizungumza na waandishi wa habari akizungumzia Sahara Sparks mwaka huu ambao inatarajiwa kufanyika tarehe 27 na 28 Semptemba mwaka huu.

 Mtambalike amesema kwa kipindi cha miaka 9 ya kuwepo sahara wamebaini wabunifu wanakosa mitaji ambayo ingewasaidia katika kukamilisha kazi.

 "Katika miaka tisa yapo makampuni yamefanikiwa lakini tumeona wabunifu wanachangamoto masuala mitaji pamoja na kutokuwa na sera,lakini sera linakwenda kufanyiwa kazi na mamlaka husika"Amesema Mtambalike.

 Aidha,Mtambalike akizungumzia Sahara Sparks mwaka huu inatarajia kukutanisha wabunifu mbao watakuwa na jukumu la kujadili mipango mbalimbali ambayo itaweza kuwasaidia hapo mbeleni.

 Kwa upande wake,Samsoni mwena ambaye ni mkurugenzi wa menejimenti na maarifa kutoka Tume ya Sayansi na teknolojia(COSTECK) amesema kwa kipindi cha miaka tisa COSTECH  wamekuwa wakishiriana na Sahara kuandaa tukio hilo na kuwayataka makampuni kuja kushudia bunifu mbalimbali.

 "Natoa wito kwa wanaofadhili wajitokeze kuja kuona bunifu mbali"Amesema Mwena ambaye pia alimwakilisha mkurugenzi wa COSTECK.


0/Post a Comment/Comments