RAIS RUTO ATANGAZA BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI.


*******

Rais William Ruto ametangaza mawaziri kumi na moja kati ya 22 katika baraza lake la mawaziri.

Katika hotuba yake kwa taifa , rais Ruto amesema kwamba idadi ya mawaziri waliosalia itatangazwa wiki ijayo baada ya mashauriano.

Haya yanajiri baada ya shinikizo kuongezeka kwa Rais kuchagua watu wenye uwezo ambao watamsaidia kutekeleza ajenda yake.

Rais amesema kwamba uteuzi huo ambao ni pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali - unafuatia mashauriano katika sekta ya kisiasa katika jaribio la kurudisha amani na utulivu nchini.

0/Post a Comment/Comments