***********
Wizara ya Fedha kama Wizara muhimu katika maendeleo ya Taifa na ufanikishaji wa Maazimio ya Dira ya Taifa ya Maendeleo Nchini, imekutana na Kamati ya usimamizi wa Dira. Wajumbe wa Tume ya Mipango na Timu ya kitaalamu na uandishi wa dira ya Maendelo 2050 , kuweza kupata picha kamili ya walipotoka na wanapokwenda
Mkutano huo uliongozwa na Waziri wa fedha Mh. Mwigulu
Nchemba pamoja Ndugu Laurence Mafuru ambaye ni Katibu Mtendaji wa Tume ya
Mipango kujadili mipango ya maendeleo na nini kifanyike kuelekea kufikia mwisho
wa ukusanyaji maoni na uandishi wa Dira 2050.
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeanza kuratibu
maandalizi ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Serikali inatambua kuwa, maono na maratajio ya watanzania na
mbinu za kuyafikia zinatokana na watanzania wenyewe kupitia ushirikishwaji
madhubuti katika maandalizi na utekelezaji wa mipango ya maendeleo.
Ili kuhakikisha Dira
hiyo inabeba maono na matarajio ya watanzania kwa miaka 25 ijayo, ni muhimu
wananchi na wadau wote wa maendeleo kushirikishwa kikamilifu katika mchakato wa
maandalizi ya Dira tangu hatua za awali hadi kukamilika kwake.
Taarifa watakazotoa zitatumika katika maandalizi ya Dira na
hivyo unahakikishiwa usiri wa taarifa watakazozitoa..
Nia na Malengo ya
kikao hiki ni kungalia mambo Muhimu ambayo
matarajio yetu kama Nchi yaliweka na kuangalia kama yalifikiwa na
kuangalia Sasa kule tunakokwenda na yale.tunayoyachukua kuendelea nayo mbele .
Mafuru alisema pia kuwa kundi hili la wataalam ni kundi la
kufikiri tulikotoka na tiunakikwenda. . Lakini pia kikao hiki kinalenga Sasa
kuangalia matarajio haya na mawazo ambayo tunaenda kuyakamilisha kuyakusanya
kutoka kwa wananchi yanalingana na maono ya Mipango ambao tunakwenda kujiwekea.
Hata Sasa tunapokwenda kuangalia maoni tunatakiwa kuwa na sura halisi ya uchumi
sanjari na Malengo ambayo tutataka kiyanona yakifikiwa. .
Na sisi kama tume pekee bila wizara hatuwezi kusonga mbele .
Hivyo basi tumekuana ili kujadili Kwa kina na kujiwekea mkakati na Malengo
ambayo si yakufikirika lakini kutekelezeka


Post a Comment