TAKUKURU KINONDONI YABAINI MAPUNGUFU KATIKA MIRADI 26

Naibu Mkuu wa TAKUKUKU (M) Kinondoni Elizabeth Mokiwa wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam akitoa taarifa ya utendaji kazi kwa kipindi cha miezi mitatu kuanzia Mwezi April hadi Juni mwaka huu.

.....................

NA MUSSA KHALID

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Kinondoni imebaini mapungufu michache katika miradi 26 yenye thamani ya Shilingi Bilioni 80,289,100,506.80 na kuwashauri wahusika kuyarekebisha ili miradi ikamilike kwa wakati na kwa thamani halisi.

Hayo yameelezwa leo jijini Dar es salaam na Naibu Mkuu wa TAKUKUKU (M) Kinondoni Elizabeth Mokiwa wakati akitoa taarifa ya utendaji kazi kwa kipindi cha miezi mitatu kuanzia Mwezi April hadi Juni mwaka huu.

Aidha Mokiwa amesema pia katika kipindi hicho TAKUKURU imepokea jumla ya malalamiko 88 ambapo 32 yamehusu rushwa na huku yasiyohusu rushwa yakiw ani 56.

Kuhusu malalamiko hayo amesema yasiohusu rushwa walalamikaji wengine wameshauria na majalada kufungwa na wengine wameelekezwa sehemu sahihi ya kupeleka malalamiko yao huku yanayohusu rushwa majalada yakiendelea kushughulikiwa.

‘Katika kipindi husika tumefungua mashauri mapya kumi na sita katika mahakama ya Wilaya ya Kinondoni na Jamhuri imeshinda mashauri mawili na mashauri 31 yanaendeelea mahakamani’.amesema Mokiwa

Naibu Mkuu wa huyo TAKUKUKU (M) Kinondoni amesema katika uzuiaji wa Rushwa kwenye kipindi hicho wamefuatilia miradi sita yenye thamani ya Shiling Bilioni nane hamsini na sita laki nane sitini elfu mia sita sabini na mbili senti sitini na saba ambapo wamebaini mapungufu machache na hivyo wamewashauri wahusika kurekebisha mapungufu hayo.

Miradi hiyo ni pamoja na mradi wa kituo cha Afya Kinondoni, mradi wa ujenzi wa barabara

ya nyota njema kunduchi, mradi wa uboreshaji wa huduma za maji safi DAWASA – Wazo,Mradi wa Vikundi vya usafi na utunzaji wa mazingira katika Manispaa ya Kinondoni, Ujenzi wa Boksi Kalavati eneo la stop over, katika Wilaya ya Ubungo na mradi wa ufungaji pampu ya maji Kibamba Kisarawe katika Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.

Katika hatua nyingine Mokiwa amesema kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa 2024 wamejipanga kuelimisha wananchi wajue madhara ya rushwa na wahamasike kushirikiana na Takukuru kutokomeza rushwa kuanzia sasa hadi wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi.

‘Rushwa katika uchaguzi hupelekea kuchaguliwa kwa viongozi wasio kuwa waadailifu watakaotumia muda wao mwingi wa uongozi kurejesha fedha zao na sio kuleta maendeleo kwa wananchi’amesema Mokiwa

Vilevile amesema katika mwaka 2023 hadi 2024 wametekeleza Program ya TAKUKURU Rafiki kwa kuwafikia wananchi kwenye kata 20 na kupokea kero 61 na kuzitatua kwa uharaka ili zisiwaathiri wananchi.

Pia amesema kuwa wameshirikiana na wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa dini,Taasisi zisizo za kiserikali,sekta ya Afya,Nishati na Maji katika kufikisha elimu ya mapambano dhidi ya rushwa kwa wananchi na kushiriki katika maonyesho na makongamamo.

Hata hivyo Taasisi hiyo imesema itaendelea kupokea malalamiko yote yanayohusu rushwa na kuyafanyia kazi kwa uharaka ili kuweza kudhibiti vitendo hivyo.

0/Post a Comment/Comments