TIB KUWAPA MIKOPO WAKULIMA KUANZIA MILIONI 50


 *******

 Ili kuongeza tija na kukuza uzalishaji katika sekta ya Kilimo nchini, Benki ya Maendeleo ya TIB inatoa Mikopo kwa wakulima kuanzia shilingi Milioni 50 hadi kufikia shilingi Biloni 2 kwariba ya asilimia kuanzia asilimia 4, hadi asilimia 8 kiwango ambacho nichachini ukilinganisha na Mikopo inayotolewa na taasisi zingine za kifedha

Meneja usimamizi wa Kilimo kutoka TIB Bi. Monica Mzilu amesema hayo katika kilele cha maonesho ya Nanenane yaliyofanyika Jijini Dodoma kuwa, Mikopo hiyo inatolewa chini ya Mfuko wa Kilimo ambao unatoa mikopo kwa wakulima wakubwa, wakati na wakulima wadogo kwalengo la kuhakikisha kuwa wanakuza sekta nzima ya kilimo na mnyororo wa thamani katika sekta hiyo

” mikopo hii inawahusu wakulima wote, wafugaji, Uvuvi lakini pia wafanyabiashara kwenye sekta hii ya Kilimo, hivyo niwahimize wakulima kujitokeza kutumia Mikopo hii kukuza shuguli zao” amesema

Aidha amesema, Benki hiyo ina mfuko unaotoa mikopo inayotolewa kwa wakulima kuanzia shilingi milioni 50 hadi bilioni 2 kwa makampuni kwa riba ya asilimia tano na vikundi vilivyosajiliwa kama saccos au 'association' kuanzia milioni 50 mpaka bilioni moja kwa riba ya asilimi nne tu ili waweze kukopesha kwa wakulima wadogo kwa riba isiyozidi asilimia nane.

"Tunatoa  mikopo hiyo yote kwenye mnyororo wa thamani wa  kilimo yaan  kuanzia mwanzo hadi kwenye masoko  ,kwa maana kwamba   tunatoa mkopo kujenga maghala au kununua vifungashio au kama mtu anataka kuchakata mazao ili kuongeza thamani ili mradi wazo husika likidhi vigezo ."

Mbali na hilo, pia TIB Wamekuwa wakitoa  elimu kwa wakulima kuhusu fursa zilizopo katika benki hiyo  kwenye maeneo tofauti hivyo kuwahimiza wakulima kutembelea mabanda yao kunapokuwa na maonesho mbalimbali mfano katika maonesho ya sabasaba na Nanenane .

Bi Mzilu pia amesema kuwa TIB imekuwa ikitoa elimu na kuwatembelea wakulima na kuwaelimisha wafahamu wanachokitaka lakini pia wanawaelimisha jinsi ya kutunza fedha na masuala mbalimbali ya biashara

Wakulima, Wavuvi na Wafugaji wanahimizwa kutembela ofisi za Benki hiyo zilizopo katika kanda zote nchini, Mwanza, Mbeya, Dar es Salaam na Arusha


0/Post a Comment/Comments