WANANCHI WANAOPISHA MIRADI NI HAKI YAO KUPATA FIDIA YA RASLIMALI ZAO

......................

Na Magrethy Katengu Dar es salaam

Tanzania inafanya jitihada za kuhakikisha Wananchi wake wanapatiwa haki raslimali katika maeneo ambayo yanapitiwa na miradi ikiwemo ya wawekezaji au serikali ili kusaidia kuondoa malalamiko kutoka kwa Wananchi.

Hayo yamesemwa Agost 29,2024 Jijini Dar es salaam na Kamishana wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Nyanda Shuli, katika Mdahalo ulioandaliwa na taasisi ya Haki raslimali ambapo amesema tume hiyo imekuwa ikifanya kazi na wadau mbalimbali ikiwemo kituo cha Sheria na haki za Binadamu(LHRC) na imekuwa ikipokea malalamiko ya aina tofauti tofauti kutoka kwa Wananchi nakuyaripoti Mahakamani kupatiwa utatuzi.

Katika Mdahalo huo wa walijadili kwa kina namna sheria zinavyoweza kumsadia mwananchi kupata haki zake pale mradi unapopita katika eneo lake aliowe fidia kulingana na hali halisi ya mali zilizopo

"Kuna baadhi ya mikanganyiko inayotokea wengine kutoridhika na fidia wanazolipwa hivyo kuamua kupeleka malalamiko mahakamani,hivyo inatakiwa elimu iendelee kutolewa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali"amesema Shuli

Kwa upande wake Mwakilishi kutoka Mradi wa Bomba la Mafuta Gafi kutoka Unganda hadi Tanzania(ECOP) Fatma Msumi amebainisha kuwa baadhi ya maeneo ambayo bomba hilo limepita Wananchi wamepatiwa stahiki zao kwa mujibu wa sheria za haki za Binadamu.

"Vingine ilitulazimu kukutana na wazee wa kimila kwanza kuzungumza nao kutokana na baadhi yao imanani zao na matambiko yao hufanyika kwenye makaburi au miti hivyo wengine kukataa kabisa kuhamisha makaburi yao na kuwalazimu wao kuangalia namna ya kukwepa maeneo hayo ili kusitokee mkanganyiko' amesema

Nakuongeza kuwa "Kiukweli Mradi huu wa bomba la mafuta Ghafi la Afrika Mashariki kila maeneo ramani yake imeonyesha litapita kuna ofisi ambayo watumishi wake wamekuwa wakizungumza na viongozi wa kijiji, kitongoji ,kimila kuweka mazungumzo ya pamoja kuhusu raslimali zao kama kuna uwezekano wa kulipwa fidia wapishe maradi "

Kwa upande wake Mtaalamu wa masuala ya haki za binadamu kutoka kituo cha Sheria na haki za binadamu LHRC Joyse Komanya amesema kituo hiko kimekuwa kikipokea malalamiko ya ukiukwaji wa haki za binadamu haki raslimali kwa wanaopisha miradi kwani wengine hulipwa fidia ndogo ikilinganishwa na mali walizonazo hivyo nao wamekuwa wakiwasaidia kwa kuwapatia Elimu namna ya kupata haki zao

 

0/Post a Comment/Comments