16 WAFARIKI HUKU 86 WAKIJERUHIWA AJALI YA GHOROFA KUPOROMOKA

 Waziri Mkuu Majaliwa akizungumza katika hafla ya kuaga miili ya waliopoteza maisha kutokana na kuporomoka kwa jengo hilo mapema Jumamosi, inayofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

............................

NA MUSSA KHALID

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa amesema amesema watu 16 wamefariki na wengine 86 wameokolewa katika ajali ya ghorofa lililoporomoka Kariakoo 

Waziri Mkuu Majaliwa amesema hayo katika hafla ya kuaga miili ya waliopoteza maisha kutokana na kuporomoka kwa jengo hilo mapema Jumamosi, inayofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Amesema kwa maelekezo ya serikali inaendelea kugharamia matibabu ya wahanga wote na hakuna anayetozwa huku waliofariki serikali inagharamia miili yote ya marehemu mpaka katika nyumba zao za mwisho.

“Mpaka sasa serikali imechukua hatua mbalimbali ikiwemo kuwezesha upatikanaji wa mitungi ya gesi kwa watu waliopo chini,kutafuta vitendea kazi kwa ajili ya watu wanaofanya uokozi”Waziri Mkuu Majaliwa

Aidha Waziri Mkuu Majaliwa amesema serikali imeunda tume ya watu 19 ambayo itafanya kazi ya kuyapitia majengo yote ya Kariakoo ili kujua ubora wa majengo hayo na shughuli zinazoendele kwani mahitaji ya soko hilo bado yapo palepale.

Awali akizungumza Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu) William Lukuvi amesema uchunguzi wa awali juu ya kuporomoka kwa jengo hilo unaendelea kufanywa huku akisisiza wadau kutoa michango yao kwenye akaunti maalum.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amesema yupo tayari kuwajibika na kwamba cheo alichonacho siyo mali kuliko uhai wa watu iwapo itabainika kuwa hakuwajibika kikamilifu katika uokozi wa jengo lililoporomoka Kariakoo.

Naye Mbunge wa Ilala na Naibu Spika wa Bunge la Tanzania,Mussa Hassan Zungu amesema Taifa limepoteza watu muhimu huku akishukuru namna wananchi wa Ilala walivyojitoa na kusimama na Taifa kukabili tukio hilo

0/Post a Comment/Comments