MAJALIWA KUONGOZA KONGAMANO LA UWEZESHAJI DODOMA DISEMBA

*****

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Majaliwa Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye kongamano la nane la uwezeshaji wananchi kiuchumi linalotarajiwa kufanyika Disemba 3 na 4 mwaka huu mkoani Dodoma.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kuhusiana na kongamano hilo Katibu wa baraza la taifa la uwezeshaji wananchi kiuchumi Beng'i Issa amesema kongamano hilo linatarajiwa kukutanisha wadau takribani 700 kwa lengo la kujadili fursa mbalimbali zinazotolewa na taasisi za serikali

Kadhalika amesema kongamano hilo lililobebwa na Kauli mbiu isemayo “Uwezeshaji wananchi kiuchumi ni msingi wa maendeleo ya watanzania” litatoa fursa ya kuwakutanisha wafanyabiashara kutoka maeneo mbalimbali ili kuweza kubadilishana ujuzi na kupeana fursa za kiuchumi.


0/Post a Comment/Comments