SERIKALI YASHAURIWA KUBORESHA SERA NA KODI KWA BIASHARA


                                            **********

Serikali imeshauriwa kuzingatia na kuimarisha mazingira wezeshi ya sera na kodi ili kukuza mapato ya serikali na kuendeleza ukuaji wa biashara nchini.

Ushauri huo umetolewa na  Mkurugenzi wa Mahusiano wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Breweries Ltd (SBL), John Manyanja, wakati wa ziara ya Kamati ya Bunge ya Wizara ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Uvuvi katika kiwanda chao kilichopo Chang'ombe jijini Dar es Salaam .

Manyanja amesema kuwa punguzo la ushuru linaacha pengo la ushuru wa asilimia 32 ikilinganishwa na bia inayotengenezwa kutoka shayiri inayooagizwa kutoka nje, ambayo inatozwa ushuru wa shilingi 918 kwa lita. Watengenezaji wa bia wanaoagiza kutoka nje wanakabiliwa na gharama za ziada za kulipia ushuru wa uagizaji na athari za mabadiliko ya thamani ya fedha za kigeni.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo, Deo Mwanyika, amesema kuwa wamesikiliza changamoto, hasa za kikodi, na watakikisha wanafikishia serikali ili kutatuliwa.

Naye Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Exaud Kigahe, amesema kuwa serikali itahakikisha inatengeneza mazingira wezeshi ili kusaidia wawekezaji wa viwanda na biashara kufanya kazi kwa ufanisi.

Kamati hiyo inatarajia kukutana na wadau tena kutoa muongozo ili kuhakikisha mazingira yanayofaa kwa ajili ya maendeleo ya sekta ya ndani, ambayo yatawezesha mabadiliko ya kiuchumi ya Tanzania na kusaidia kujenga uchumi wa kujitegemea na wenye ustahimilivu.






















Picha mbalimbali wakati wa ziara ya Kamati ya Bunge ya Wizara ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Uvuvi katika kiwanda  cha Kampuni ya Bia ya Serengeti Breweries Ltd (SBL), kilichopo Chang'ombe jijini Dar es Salaam



 


0/Post a Comment/Comments