Hayo ameyasema jana jijini dar es salaam na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha
Elijah Mwandumbya akimwakilisha Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba kwenye Mahafali
ya kumi na saba kwenye chuo cha kodi (ITA) ambapo wamehitimu jumla ya wahitimu
417.
Elijah amesema Chuo kijikite na tafitia ambazo zitatoa suluhu za changamoto
kwenye mfumo wa ukusanyaji wa kodi huku mapendekezo mengi kwenye tafiti
yanakosa utafiti kwenye jamii hivyo yataleta mapendekezo na tafiti kwenye
kufikia malengo wanayoyataka.
Aidha Elijah Amewasisitiza Chuo kiendelee kutoa mafunzo ya viwango vya juu
kuzingatia kasi ya maendeleo ya sayansi na teknolojia kwani ndipo dunia
inapoelekea kwa sasa.
Kwa upande wake Kamishna Mkuu wa Kodi Tanzania (TRA) Yusuph Mwenda amesema
baraza lililopo liendelee kufanya kazi ili kufanikisha watumishi ambapo
itawezesha kuongeza idadi ya walipa kodi pamoja na kuongeza ulipaji kodi kwa
nchi na wataendelea kuboresha miundombinu ili watoe wahitimu bora kwa maendeleo
ya nchi.
"Dhamira ya Chuo cha Kodi ni kukifanya kuwa cha kimataifa chenye kutoa wahitimu wabobezi katika masuala ya Forodha na Kodi" amesema Mwenda.
Naye, Mkuu wa Chuo
hicho,Profesa Isaya Jairo amesema Chuo kimetengeneza wataalamu wengi wa forodha
na kodi kwenye misingi ya kujenga umahiri na kukuza uchumi wa Taifa
pamoja na kutumia fursa za uendeshaji wa teknolojia na sayansi na itasaidia
wahitimu hao waendane na kasi ya teknolojia na forodha ya dunia ya sasa.
Amesema pia kimekuwa kikitumia fursa za uendeshaji wa teknolojia na sayansi kwa sasa ambayo itawasaidia wahitimu hao kuendana na dunia ya sasa
Chuo hicho kimetunuku vyeti kwa wahitimu 417 wa kozi mbalimbali kwa mwaka wa masomo 2023/2024 huku idadi hiyo wanaume ni 236 na wanawake 181 ambapo195 wametunukiwa cheti cha Uwakala wa forodha wa Afrika Mashariki(EACFF),Wahitimu 28 wametunukiwa Cheti cha Usimamizi wa Forodha na Kodi (CCTM),

Post a Comment