TBS YAWATAKA WAZALISHAJI KUWEKA TAARIFA MUHIMU KWENYE BIDHAA ZAO

Afisa Udhibiti Mkuu wa ubora,kutoka  Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Mosses Mbambe wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo Nov 26,2024  akizungumzia umuhimu wa uwekaji taarifa kwenye bidhaa na umuhimu kwa watumiaji kusoma taarifa zilizopo kwenye vifungashio kabla ya kuzitumia.

......................

NA MUSSA KHALID

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limewasisitiza watumiaji wa bidhaa mbalimbali nchini wazisome taarifa zake kabla ya kununua ikiwemo kuangalia mwisho wa matumizi ili kujiepusha na athari zinazoweza kujitokeza baada ya kuzitumia.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Afisa Udhibiti Mkuu wa ubora,kutoka  Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Mosses Mbambe wakati akizungumza na waandishi wa habari  akizungumzia umuhimu wa uwekaji taarifa kwenye bidhaa na umuhimu kwa watumiaji kusoma taarifa zilizopo kwenye vifungashio kabla ya kuzitumia.

Mbambe amesema kuwa suala la uwekaji taarifa kwenye bidhaa lipo kwa mujibu wa sheria lakini pia linaongozwa na viwango vya bidhaa husika hivyo amewasisitiza wazalishaji kuweka taarifa hizo kwani zinasaidia mawasiliano baina ya mzalishaji na watumiaji.

Aidha Afisa Udhibiti huyo amesema kuwa ni vyema watumiaji wakasoma kwa umakini tahadhari ambazo zinatolewa na wazalishji wa bidhaa ili kuepuka madhara ya kiafya yakiwemo ya alegi ambayo yanaweza kuwapata.

 “Kwa bidhaa ambazo zimewekewa muda wa kuisha kwa matumizi mfano expire date tumezoea pia kuona use by date na best before hizi ni lugha ambazo zinatumiwa kwenye bidhaa mbalimbali na ukikuta bidhaa imeandikwa expire date hiyo inapaswa kuondolewa kwenye soko ukikutana nazo kwenye soko ni vyema mtumiaji ukatoa taarifa mapema ili Shirika liweze kudhibiti’amesema Mbambe

Hata hivyo TBS imewataka watanzania kutoa taarifa pindi wanapokutana na bidhaa ambazo zimekwisha muda wake kwenye soko ili Shirika lifuatilie na kuweza kufanya udhibiti kwa wakati.

0/Post a Comment/Comments