DKT. BITEKO ATAKA WATAFITI, WABUNIFU NDANI YA NCHI WATAMBULIWE KULETA MAENDELEO

 ]

*******

 Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema umefika wakati kwa Serikali na taasisi na Mashirika kutambua, kuthamini na kutumia tafiti za wanasayansi wa ndani ya nchi ili kutatua changamoto zilizopo.

DKt. Biteko amemsema hayo leo Disemba 2, 2024 wakati akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kufungua Kongamano la tisa la Sayansi, Teknolojia, Ubunifu na maonesho linaloendelea Jijini Dar es Salaam.

Amesema wanasayansi nchini wanafanya kazi nzuri na kubwa ya kutafuta suluhu ya matatizo mbalimbali katika jamii lakini kazi zao zinatambuliwa zaidi nje ya nchi kuliko zinavyotambuliwa nchini jambo ambalo linaweza kuwavunja moyo.

“Kongamano hilo ni la kujadili na kutafuta suluhu ya matatizo tuliyonayo, tutumie tafiti za wanasayansi wa ndani badala ya kuwavunja moyo na kila anayejaribu kwa kutafiti apewe fursa ili aendelee kutafiti zaidi na matokeo tutayaona,” amesema DKt. Biteko.

Ameongeza kuwa Serikali inatambua mchango wa wanasayansi na kuwawezesha watafiti na wabunifu na kupitia Tume  ya Sayansi na Teknolojia COSTECH imetoa kiasi cha bilioni 32 kwa ajili ya kuimarisha miradi ya utafiti na ubunifu.

Tangu mwaka 2015 Serikali imeshapokea kiasi cha shilingi bilioni 222.8 kwa ajili ya kujenga uwezo kwa wanasayansi wabunifu kuendeleza miradi mbalimbali ambazo zimesaidia kuwajengea uwezo wanasayansi wakiwemo wanasayansi vijana.






0/Post a Comment/Comments