DKT MWIGULU ALAANI SHAMBULIZI WATUMISHI TRA


.....................

Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba amesema amesikitishwa na tukio la kushambuliwa kwa Watumishi watatu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na gari lao (STL 9923) walipokuwa wakitekeleza majukumu yao ya kisheria ya kudhibiti magendo na magari yaliyoingizwa nchini kinyume cha sheria, usiku wa December 5, 2024, katika eneo la Tegeta kwa Ndevu, Dar es Salaam.

Taarifa iliyotolewa na Waziri Mwigulu leo December 06,2024 imesema “Watumishi hao walikuwa wakifuatilia gari namba T229 DHZ (BMW X6) lililoingizwa nchini bila kulipa kodi stahiki, natoa kwa wote waliojeruhiwa na kuwaombea wapate nafuu haraka”

“Wizara ya Fedha inalaani vikali tukio hili na kuahidi kuwa hatua kali zitachukuliwa dhidi ya wahusika wa uhalifu huu, aidha TRA itaendelea kutekeleza majukumu yake kwa weledi na kwa mujibu wa sheria”

0/Post a Comment/Comments