KCB BANK YADHAMINI TIMU YA GOFU YA LUGALO MASHINDANO YA AFRIKA MASHARIKI

 

******

Msafara wa watu saba wa timu ya mchezo wa gofu ya Lugalo Dar es Salaam imeondoka nchini kuelekea Nairobi Kenya kwaajili ya kushiriki mashindano ya Afrika Mashariki yatakayoanza kutimua vumbi Disemba saba mwaka huu.

Mkuu wa msafara wa timu ya gofu ya Lugalo Meja Jenerali Ibrahim Michael amekabidhiwa bendera na wadhamini wa timu hiyo benki ya KCB ili kuanza safari hiyo kuelekea Kenya

Amesema wachezaji wake wapo tayari na anaamini watarudi na ubingwa wa michuano hiyo ya Afrika Mashariki

Kwa upande wake Mwakilishi kutoka benki ya KCB Bi Frida Shirima amesema benki hiyo itaendelea kuunga mkono sekta ya michezo kwa maslahi mapana ya Taifa.

Jumla ya timu 10 kutoka nchi za Afrika Mashariki zimekata tiketi ya kushiriki katika mashindano hayo baada ya kufanya vizuri kwenye nchi zao huku Mashindano hayo yatafanyika kwa muda wa siku mbili na yataanza kutimua vumbi Ijumaa na kumalizika Jumamosi wiki hii







0/Post a Comment/Comments