MAWAKALA WA FORODHA WAPEWA MIKAKATI YA KUFANYA KAZI KATIKA MPAKA SIRARI

Picha ya pamoja Mkuu wa Wilaya ya Tarime Meja Edward Gowele pamoja na Taasisi za Serikali zinazofanya katika mpaka wa Sirari ,Mawakala wa Forodha

********

Na Mwandishi Wetu

Mkuu wa Wilaya ya Tarime Meja Edward Gowele amewataka mawakala wa Forodha katika Mpaka Sirari kuzingatia sheria katika kufanya kazi mpakani hapo.

Meja Gowele ameyasema hayo wakati akizungumza katika mkutano wa Mawakala wa Forodha uliondaliwa na Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania TASAC uliofanyika katika Ofisi za TRA Sirari wilayani Tarime mkoani Mara.

Amesema kuwa Sheria zipo ambazo zinaongoza kazi ya Uwakala  wa forodha hivyo lazima zifuatwe katika kuendelea  nchi kupata mapato kwa ajili ya maendeleo  mbalimbali.

Meja Gowele amesema kuwa mawakala wa Forodha wanatakiwa kuwa na ofisi ambazo zitasaidia TASAC kuwafikia na wakati changamoto  zinapotokea kufanya urahisi wa kuzitatua.

Amesema kuwa kutokana na changamoto  zinazojitokeza kwa kuwa na mawakala ambao hawajasajiliwa amewataka kuwa na vitambulisho ambavyo watatumia katika kufanya kazi katika eneo la mpaka wa Sirari kati ya Tanzania na Kenya.

Hata hivyo amesema katika mpaka huo kuna watu wanafanya uwakala wa forodha  hawajasajiliwa na kufanya kuharibu taswira kwa watu waliopo kisheria ambapo mapato yao yanapotea kutokana na kuwa na hao mawakala wasiosajiliwa.

Mtakwimu Mwandamizi wa TASAC Athman Athman amesema kuwa mawakala wa forodha sheria ziko wazi katika kufanya kazi hiyo na wasipofuata sheria hatua zinachukuliwa.

Amesema kuwa katika kuhakikisha mawakala wanaotoa huduma za forodha TASAC kazi yake kutoa elimu katika kuwa na mawasiliano ambayo yanaboresha kazi zao.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Uwakala wa Forodha  ya Emaus Logistics Tanzania Limited  Maryam Muhambo amesema changamoto zinatokana katika Mawakala wa Forodha ni elimu na kuiomba TASAC kufanya kikao na Viongozi Chama Mawakala wa Forodha  Tanzania (TAFF) ambao watakwenda kutoa elimu kwa wananchama wao.

Maryam amesema kuwa misingi ya kufanya kazi za uwakala wa forodha hivyo kazi ya mawakala ni kufuata ili kuepusha migongano na Taasisi za Serikali zinazodhibiti kazi hiyo.

Nae Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji katika Mpaka wa Sirari Deodatus Sanda amesema kuwa mawakala wataofanya udanganyifu watachukuliwa hatua.

Amesema ujirani mwema uliopo kati ya Tanzania na Kenya uendelee kwa watu kutembea kilomita 10 kwa kila nchi na nje hapo hatua zitachukuliwa.

Amesema kwa madereva wanaoingia na magari biashara wanatakiwa kulipa na sio kutumia ujirani mwema wa kutembea kwa miguu.

Kaimu Meneja wa Forodha wa TRA Abdallah Salum amesema kuwa kazi wanaendelea kushirikiana na mawakala wa Forodha kufuata taratibu za kulinda mawakala wa Forodha  kwa kutoruhusu watu wengine wasiokuwa na utalaam kufanya kazi hiyo.

Picha ya pamoja Mkuu wa Wilaya ya Tarime Meja Edward Gowele pamoja na Taasisi za Serikali zinazofanya katika mpaka wa Sirari ,Mawakala wa Forodha.
Mtakwimu Mwandamizi  wa TASAC ,Athuman Athuman akizungumza kuhusiana na matakwa ya Sheria ya Uwakala wa Forodha kwa mawakala wa Forodha Sirari mpaka  wa Tanzania na Kenya.

0/Post a Comment/Comments