Kutokana na leseni hiyo, Torch Media
sasa itaanza kurusha maudhui hayo wakati wowote kwa lengo la kuhabarisha jamii,
kuelimisha na kuburudisha.
Kwa mujibu wa leseni hiyo
iliyosainiwa na Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka hiyo, Dkt. Jabiri Bakari, Torch
Media itaendelea kurusha maudhui ya mtandaoni kwa kipindi cha miaka mitatu.
Aidha, maelekezo hayo yanazingatia
kifungu cha Sheria cha 2(a), 4(1) na 23(1)(c) cha Sheria ya Mawasiliano ya
Kielektroniki na Posta, sura ya 306 ya Sheria za Tanzania na sehemu ya 6 ya
Udhibiti wa Mawasiliano ya Tanzania.
Sambamba na Sheria ya Mamlaka ya
Mawasiliano, sura namba 172 R.E ya Sheria za Tanzania na Kanuni ya 4 ya
Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta, Kanuni ya mwaka 2018.
"Mwenye leseni atazingatia
masharti yote yaliyoainishwa katika leseni hii na udhibiti mwingine mahitaji
yaliyotolewa chini ya Kanuni na Kanuni zilizotolewa chini ya Sheria."
"Kadhalika, kuhakikisha watoto
wanalindwa dhidi ya ufikiaji wowote wa maudhui ambayo ni hatari kwa ustawi
wao" imeelezwa na sehemu ya leseni hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa
Torch Media, James Salvatory Gerald, ameishukuru Serikali kwa kuona umuhimu wa
kuupatia leseni mtandao wa Torch Media kurusha maudhui ya runinga.
"Nimatumaini yetu Watanzania
wataendelea kufurahia habari mbalimbali hasa za kijamii kutoka maeneo
mbalimbali ya nchi."
"Leseni hii ni chachu kubwa
kwetu Torch Media kwa maana tunakwenda kufanya mapinduzi makubwa ya kihabari
ili kuhakikisha wasomaji wetu wanapata habari bora zenye ukweli, usahihi na
ulinganifu kwa maslahi mapana ya umma."
"Tunaipongeza sana Serikali
kupitia Mamlaka ya Mawasiliano nchini kwa kuona umuhimu wa kutupa leseni mpya
ya kurusha habari kupitia runinga ya mtandaoni kwa kuzingatia masharti
mbalimbali, hakika tutaendelea kuheshimu mipaka yetu ya kihabari kwa kulinda
maadili ya uandishi wa habari," ameongeza Salvatory.
Hata hivyo, ameziomba mamlaka za
Serikali kutoa ushirikiano mkubwa kwa waandishi wa habari wa mtandao wa Torch
Media ambao wametapakaa sehemu mbalimbali za nchi, kwa kuwapa taarifa muhimu na
kwa wakati kwa manufaa mapana ya nchi.
"Nitumie nafasi hii kuziomba
mamlaka mbalimbali za nchi kuendelea kutoa ushirikiano mkubwa kwa waandishi wa
habari nchini wakiwemo wa mtandao wetu ili kuihabarisha na kuelimisha jamii
mambo muhimu yenye maslahi kwa umma."
"Leseni hii haitakuwa na maana
yoyote iwapo umma hautapata habari zenye ubora unaotakiwa, hivyo niwaombe wadau
mbalimbali watupe ushirikiano mkubwa katika kutimiza majukumu yetu jambo
litakalo saidia jamii kupata maendeleo yanayo kusudiwa," amesema Salvatory.
Mbali na hilo, amesisitiza jamii
kutumia mtandao wa Torch Media kufikisha changamoto zao sehemu zinazohusika ili
ziweze kipatiwa majibu ya haraka na Serikali pamoja na wadau wengine wa
maendeleo badala ya kulalamika na kujichukulia sheria mkononi kinyume na sheria
za nchi.
Post a Comment