WAHITIMU MZUMBE WASHAURIWA KUTOKUCHAGUA KAZI

****

MKUU wa Chuo Kikuu Mzumbe, Dkt. Ali Mohamed Shein, amewataka wahitimu wa chuo hicho kutochagua kazi wanapoingia katika soko la ajira, huku akiwakumbusha kwamba mafanikio yao kielimu yanaakisi uwezo na nafasi yao ya kufanikiwa kimaisha hata katika mifumo isiyo rasmi ya ajira.

Hayo yamesemwa na Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe , Dkt. Ali Mohamed Shein wakati wa Mahafali ya 23 ya Chuo Kikuu Mzumbe, Kampasi ya Dar es Salaam, yaliyofanyika leo Desemba 5, 2024 katika Kituo Cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

 Akizungumza katika mahafi hayo, Dkt. Shein amesema kusoma ni njia moja katika kutafuta maisha, na kwamba hakuna njia ya mkato katika mchakato huo, huku akiwapongeza kwa mafanikio waliyoyapata katika hatua hiyo kielimu na kuwatakia kila la kheiri wanapoingia katika hatua ya tatu ya ushindani kwenye soko la ajira.

 “Kusoma ni njia miongoni mwa njia katika kutafuta maisha na katika hilo hakuna njia ya mkato, nyie mshavuka katika hatua ya kwanza na ya pili kielimu na sasa mnaingia hatua ya tatu. Elimu haina mwisho, leo nawapongeza kwa juhudi kubwa, mmehangaika kusoma na hatimaye mmeweza.

 “Jitihada kubwa mmeonesha kuwa mnaweza kujipambania na hiyo ni uthibitisho kwamba mnaweza kujipambania nje ya vyuo, manweza kujipambania katika soko la ushindani wa ajira, wito wangu kwenu ni kwamba msichague kazi, msisubiri kuajiriwa serikalini, tumieni elimu kujiajiri.

 Katika hotuba yake kwenye mahafali hayo, Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Mzumbe, Profesa Saida Yahya-Othman, amewapongeza wafanyakazi wa chuo kwa kazi kubwa na adhimu wanayoendelea kuifanya ya kuwaandaa vijana, na kwamba anaamini wanaohitimu hao wako tayari kuikabili dunia na changamoto zake.

 Prof. Saida amesema “Niwapongeze wahitimu wote mtakaotunukiwa Stashahada, Astashahada na Shahada leo, juhudi na uvumilivu mliouonesha kipindi chote cha masomo yenu, hakika zinawastahilisha vyeti mnavyopokea leo.

 “Tunaposherehekea mafanikio ya kuhitimu masomo yetu, tufanye tafakuri ya maisha yetu ya chuoni na yale ya baadae, na changamoto zitazotukabili katika soko la ajira, na katika maisha yetu kwa ujumla. Changamoto ni nyingi, na zimeathiri kwa kiasi kikubwa mfumo wa kiutendaji na ajira.


Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Dkt. Ali Mohamed Shein, akizungumza wakati wa Mahafali ya 23 ya Chuo Kikuu Mzumbe yaliyofanyika katika Kituo Cha Mikutano cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam leo Novemba 05, 2024.









Matukio mbalimbali katika wakati wa Mahafali ya 23 ya Chuo Kikuu Mzumbe yaliyofanyika katika Kituo Cha Mikutano cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam leo Desemba 05, 2025.

0/Post a Comment/Comments