WATU 174 WAFARIKI DUNIA KATIKA AJALI YA NDEGE KOREA KUSINI

Watu 174 wamepoteza maisha katika ajali mbaya zaidi ya ndege katika historia ya Korea Kusini baada ya ndege ya shirika la Jeju Air kuanguka wakati ilipokuwa inatua na kuwaka moto katika uwanja wa ndege wa Muan.

Kulingana na wizara ya uchukuzi ya Korea Kusini, ndege hiyo ya shirika la Jeju Air, chapa 7C2216, ikitokea mji mkuu wa Thailand, Bangkok, ikiwa na abiria 175 na wafanyikazi sita wa ndege, ilijaribu kutua katika uwanja huo uliopo kusini mwa nchi mapema asubuhi.

Wafanyikazi wawili wa ndege wameokolewa wakiwa hai, huku maafisa wakieleza kuwa wengine wote waliobaki huenda wamefariki.

Ajali hiyo ya ndege katika ardhi ya Korea Kusini pia inatajwa kuwa mbaya zaidi iliyohusisha shirika la ndege la Korea Kusini katika muda wa takriban miongo mitatu, kulingana na wizara ya uchukuzi.

Ndege aina ya Boeing 737-800 yenye injini mbili ilionekana katika video zilizochapishwa kwenye vyombo vya habari vya nchi hiyo ikianguka kabla ya kugonga ukuta na hatimaye kuwaka moto.


 

0/Post a Comment/Comments