Kulingana na wizara ya uchukuzi ya Korea Kusini, ndege hiyo ya shirika la Jeju Air, chapa 7C2216, ikitokea mji mkuu wa Thailand, Bangkok, ikiwa na abiria 175 na wafanyikazi sita wa ndege, ilijaribu kutua katika uwanja huo uliopo kusini mwa nchi mapema asubuhi.
Wafanyikazi wawili wa ndege wameokolewa wakiwa hai, huku maafisa wakieleza kuwa wengine wote waliobaki huenda wamefariki.
Ajali hiyo ya ndege katika ardhi ya Korea Kusini pia inatajwa kuwa mbaya zaidi iliyohusisha shirika la ndege la Korea Kusini katika muda wa takriban miongo mitatu, kulingana na wizara ya uchukuzi.
Ndege aina ya Boeing 737-800 yenye injini mbili ilionekana katika video zilizochapishwa kwenye vyombo vya habari vya nchi hiyo ikianguka kabla ya kugonga ukuta na hatimaye kuwaka moto.
Post a Comment