*****
Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), limepongeza viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) waliochagulia na kuteuliwa katika nyadhifa mbalimbali.
Mapema jana chama hicho katika Mkutano wake Mkuu Maalum ilimteua Samia Suluhu Hassan kuwa mgombea wa Urais na Dk Balozi Emmanuel Nchimbi kuwa mgombea wake mwenza.
Aidha, Dk Hossein Ali Mwinyi ameteuliwa kuwa mgombea wa Urais kwa upande wa Zanzibar huku kada mkongwe Stephen Wassira akichagulia kuwa Makamu wa Mwenyekiti wa chama hicho Bara.
"TEF inaamini viongozi hao wataendeleza juhudi za kulipatia Taifa maendeleo na kuondokana na lindi la umaskini, " alisema Mwenyekiti wa TEF, Deodatus Balile katika taarifa yake kwa vyombo vya habari.
Post a Comment