TRUMP KUSITISHA MISAADA YA ARVs AFRIKA

Aliyewahi kuwa Waziri wa zamani wa Ardhi, Prof. Anna Tibaijuka amesema afya za Mamilioni ya Waafrika na Watanzania zipo hatarini kutokana na uamuzi wa Rais wa Marekani Donald Trump kusitisha misaada kwa Mashirika ya Afya Duniani hususani PEPFAR na GLOBAL FUND ambapo amesema uamuzi huo ukitekelezwa ni kiama.

Kupitia ukurasa wake wa X (zamani Twitter), Prof. Tibaijuka amesema “Upatikanaji wa madawa ya kuongeza kinga za mwili ARVs utaathirika, ninashauri Wizara ya Afya kuufahamisha umma wa Watanzania je ni hatua gani za haraka zinachukuliwa kutathmini jambo hili na kuchukua hatua stahiki?, ikibidi African Union waitishe kikao maalum kuangalia suala hili na kuweka mkakati wa pamoja, Waathirika wa gonjwa hili la UKIMWI ni Waafrika na ugonjwa haujulikani ulitoka wapi?, tujitetee”

Aidha amesema juhudi za kuthibiti maambukizi ya virusi vya UKIMWI ziwekewe nguvu mpya, upatikanaji wa ARVs utakuwa mgumu na kununua ARVs kibiashara ni jambo litakalohitaji bajeti kubwa na uwezo wa taifa kwa ujumla ni mdogo na jambo limekuwa la ghafla, Waathirika wengi hawana uwezo kununua madawa hayo wenyewe maisha yao yote”

“Afya zao zikidhoofika itatumika gharama kubwa kuwauguza hivo kusababisha umaskini na vifo, pia bila ARVs maambukizi yatashika kasi mpya, tuwe macho”amesema Tibaijuka



 



0/Post a Comment/Comments