Tausi Mbowe
Wanafunzi wa Chuo cha Afya cha Paradigms College wametembelea Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania (TMDA).
Wanafunzi hao walitembelea ofisi hizo Kanda ya Mashariki.
Ziara hiyo imefanyika leo Ijumaa Januari 24, 2025 katika ofisi za mamlaka hiyo zilizopo jijini Dar es Salaam.
Pamoja na mambo mengine, wanafunzi hao wamejifunza mambo mbalimbali ikiwamo udhibiti, usimamizi na ubora wa Dawa , Vifaa Tiba na Vitendanishi.
Pia walitembelea maabara ya Mamalaka hiyo kwa ajili ya ukaguzi wa Dawa na Vifaa Tiba pamoja na vitwndanishi.
Post a Comment