MRADI WA MATENKI YA MAFUTA KIGAMBONI WAFIKIA ASILIMIA 14.77, KUONDOA CHANGAMOTO KWA MELI ZA MAFUTA


*******

Mradi wa ujenzi wa matenki ya hifadhi ya mafuta katika eneo la Kigamboni, jijini Dar es Salaam, umefikia asilimia 14.77. Mradi huu unajumuisha ujazaji na ushindiliaji wa kifusi ili kuwezesha uhifadhi bora wa mafuta.

Akizungumza wakati wa ziara yake kwenye mradi huo, Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa, amesema lengo la mradi ni kuondoa changamoto za meli za mafuta kusubiri kwa muda mrefu bandarini kutokana na uchache wa matenki ya hifadhi yaliyopo.

Kuhusu ufanisi wa bandari, Prof. Mbarawa amesema umeimarika, ambapo mapato ya sekta binafsi yameongezeka na kufikia wastani wa shilingi bilioni 440 katika miezi sita iliyopita. Aidha, muda wa kushusha mizigo ya makasha umepungua kutoka siku saba hadi siku tatu tangu kampuni ya DP World kutoka Dubai ilipoanza kazi.

Kwa upande wake, Kaimu Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Baraka Mdima, amesema watahakikisha mradi huo unatekelezwa kwa viwango bora.

Mradi huu unagharimu shilingi bilioni 678.76 na unahusisha ujenzi wa matenki 15. Kati ya hayo, matenki sita yatatumika kuhifadhi dizeli, matano petroli, matatu kwa mafuta ya ndege, huku tenki moja likitumika kuhifadhi mafuta ya akiba. Mradi wa ujenzi wa matenki ya hifadhi ya mafuta katika eneo la Kigamboni, jijini Dar es Salaam, umefikia asilimia 14.77. Mradi huu unajumuisha ujazaji na ushindiliaji wa kifusi ili kuwezesha uhifadhi bora wa mafuta.

Akizungumza wakati wa ziara yake kwenye mradi huo, Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa, amesema lengo la mradi ni kuondoa changamoto za meli za mafuta kusubiri kwa muda mrefu bandarini kutokana na uchache wa matenki ya hifadhi yaliyopo.

Kuhusu ufanisi wa bandari, Prof. Mbarawa amesema umeimarika, ambapo mapato ya sekta binafsi yameongezeka na kufikia wastani wa shilingi bilioni 440 katika miezi sita iliyopita. Aidha, muda wa kushusha mizigo ya makasha umepungua kutoka siku saba hadi siku tatu tangu kampuni ya DP World kutoka Dubai ilipoanza kazi.

Kwa upande wake, Kaimu Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Baraka Mdima, amesema watahakikisha mradi huo unatekelezwa kwa viwango bora.

Mradi huu unagharimu shilingi bilioni 678.76 na unahusisha ujenzi wa matenki 15. Kati ya hayo, matenki sita yatatumika kuhifadhi dizeli, matano petroli, matatu kwa mafuta ya ndege, huku tenki moja likitumika kuhifadhi mafuta ya akiba.









 




0/Post a Comment/Comments