RAIS SAMIA KIELELEZO CHA MAFANIKIO SEKTA YA MICHEZO

Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Neema Msitha  wakati akizungumza na  waandishi wa habari   jijini Dodoma leo Feb 18,2025
Baadhi ya wanahabari jijini Dododa ambao wameshiriki kwenye mkutano wa Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Neema Msitha leo feb 18,2025 
......................

Na Ester Maile _Dodoma 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekuwa kielelezo cha mafanikio makubwa yanayoendelea katika sekta ya michezo kwa kuhamasisha na kuweka mazingira mazuri ya michezo nchini.

Hayo yameelezwa leo 18/Februari 2025 na 
Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Neema Msitha  wakati akizungumza na  waandishi wa habari   jijini Dodoma.

Ameongeza kuwa, Rais Samia ameleta mabadiliko kwa vitendo ambayo yameongeza ufadhili, ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya kisasa  ikiwemo ukaranbati wa uwanja wa BENJAMIN MKAPA.

Ametaja mafanikio mengine kuwa  Tanzania imekuwa  mwenyeji wa matukio makubwa ya michezo ya Kimataifa, kuondoa kodi kwa nyasi bandia, Tanzania kuwa Makao Makuu ya Sekretarieti ya Baraza la Michezo la Afrika Kanda ya Tano na kuanzishwa kwa Mfuko wa Michezo.

Vile vile, Tanzania kushiriki mashindano ya Kombe la Dunia, kuanzishwa kwa mfumo wa usajili wa Vyama na Vilabu wa kidijitali "SARS", kufanya vizuri katika mashindano ya kimataifa pamoja na timu za Tanzania kufuzu mashindano ya kimataifa.

0/Post a Comment/Comments