SELCOM PESA YAZINDULIWA, KUTOA HUDUMA YA KIFEDHA KIDIGITALI

Benki ya Selcom Microfinance Tanzania Limited imezindua rasmi SELCOM PESA, huduma ya kifedha ya kidigitali inayolenga kutoa suluhisho rahisi, salama, na nafuu kwa Watanzania.

Kupitia teknolojia ya kisasa na mfumo wa TIPS, huduma hiyo inawawezesha watumiaji kufanya miamala ya kifedha kwa gharama nafuu, ikiwa ni pamoja na uhamishaji wa fedha kati ya benki na mitandao ya simu, malipo ya bili, na malipo ya Serikali kupitia GePG.

Uzinduzi huo ulihudhuriwa na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Emmanuel Tutuba, ambaye alisisitiza umuhimu wa teknolojia katika kuimarisha ushirikishwaji wa kifedha na kupunguza gharama za miamala kwa wananchi.

Uzinduzi huu umeambatana na kampeni maalum ya “5 kwa Jero”, inayoruhusu wateja kufanya miamala mitano kwa siku kwa Sh500 tu, hatua inayolenga kupunguza gharama za kifedha kwa wananchi wa kipato cha chini.

Huduma ya SELCOM PESA inapatikana kupitia Google Play na App Store, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Selcom Microfinance Tanzania kuleta mapinduzi katika sekta ya kifedha na kuhakikisha huduma za kifedha zinakuwa nafuu na zinazopatikana kwa urahisi kwa Watanzania wote.

 





 

0/Post a Comment/Comments