TAKUKURU KINONDONI YABAINI MAPUNGUFU KWENYE MRADI WA BILL 2

Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Kinondoni Christian Nyakizee wakati akitoa taarifa ya utendaji kazi kwa kipindi cha Octoba hadi Disemba 2024.
.....................

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Kinondoni imebaini mapungufu madogo katika miradi mwili yenye thamani ya Shilingi Millioni 144,800,000 iliyohusu sekta ya elimu na Ujenzi.

Hayo yamebainishwa leo jijini Dar es salaam na Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Kinondoni Christian Nyakizee wakati akitoa taarifa ya utendaji kazi kwa kipindi cha Octoba hadi Disemba 2024.

Nyakizee amesema katika kipindi hicho wamefuatilia miradi mitano yenye thamani ya Shs Bill 2.85 huku miwili ikikutwa na mapungufu na hivyo kuwashauri wahusika kufanya marekebisho.

‘Mradi wenye thamani ya milioni tisini ulibainika kubadilishwa kazi iliyotolewa kibali awali ambapo kilikuwa ni cha kufanya ukarabati wa majengo ya madarasa lakini badala yake wakaanzisha ujenzi wa madarasa mapya’amesema Nyakizee

Aidha Mkuu huyo wa TAKUKURU (M) Kinondoni amesema katika kipindi hicho wamepokea malalamiko 85 ambapo kati ya hayo 46 lihusu Rushwa na 39 hayakuhusu rushwa.

Amesema kuhusu malalamiko ambayo hayakuhusu rushwa walalamikaji wengine wameshauriwa na majalada kufungwa na wengine wameelezwa sehemu sahihi ya kupeleka malalamiko yao.

Katika hatua nyingine Nyakizee amesema wamejipanga kuendelea kuhamasisha wananchi kushirikiana na TAKUKURU wakati wa maandalizi ya uchaguzi Mkuu wa mwaka huu wa Madiwani,Wabunge na Rais.

‘TAKUKURU tutaendelea kupokea malalamiko yote yanayohusu rushwa na kuyafanyia kazi kwa uharaka ili kuweza kudhibiti vitendo vyote vya rushwa katika wakati wote’ameendelea kusisitiza Nyakizee

Hata hivyo imeendelea kuwasisitiza na kuwakumbusha watumishi kuzingatia misingi ya maadili ya utumishi wa umma katika kutekeleza majukumu yao bila kujihusisha na rushwa kwani inanyima haki

0/Post a Comment/Comments