TCB YAJIZATITI KUIMARISHA UCHUMI NA MAENDELEO JUMUISHI KWA JAMII

*****
Na mwandishi wetu  Dar es salaam 

Benki ya Biashara ya Tanzania (TCB) imesema kuwa itaendelea  kuwa mdau muhimu katika kuimarisha uchumi wa mtu mmoja mmoja na jamii kwa ujumla kupitia sekta mbalimbali za kijamii na kiuchumi nchini.

Akzingumza Katika hafla ya Iftari iliyofanyika  leo Machi 28, 2025 jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa TCB, Adam Mihayo, ameeleza dhamira ya benki hiyo kuwa ni  kushirikiana na Serikali katika kujenga uchumi imara.

Mihayo amesema kuwa benki hiyo imekuwa ikitoa misaada katika sekta muhimu, ikiwemo kusaidia madawati katika shule na kutoa misaada katika hospitali.

Ameongeza kuwa TCB inaendelea kupunguza mzigo kwa serikali kwa kugusa moja kwa moja sekta zinazohitaji msaada na pia kuimarisha maendeleo jumuishi kwa jamii.

Kwa uapnde wake Naibu Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Hassan Chizenga, ameipongeza TCB kwa kuandaa tukio hilo lililoweka pamoja watu kutoka makundi mbalimbali ya jamii, akisema kuwa hiyo ni mfano mzuri wa kujali na kuungana kwa jamii.

Amesema  kuwa benki hiyo inapaswa kuendelea kuigusa jamii kwa vitendo, na kuonesha kwa mfano wake ukongwe na mchango wake mkubwa katika maendeleo ya kijamii.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na watu mbalimbali, wakiwemo viongozi wa dini, watoto kutoka vituo vya kulea watoto yatima, wafanyakazi wa TCB, wateja wa benki hiyo, na jumuiya ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albinism), ikiwa ni sehemu ya juhudi za TCB kuimarisha maendeleo jumuishi na kusaidia makundi yenye uhitaji.













0/Post a Comment/Comments