MBETO AWATAKA WANA-CCM KUTETEA SERA ZA CHAMA NA KUWASEMEA VIONGOZI


 *****

Na Mwandishi  wetu, Zanzibar 

Chama cha Mapinduzi (CCM )  kimewataka makada wake, viongozi na  wanachama kutetea sera za chama , kuwalinda na kuzungumzia mafanikio ya kazi zilizofanywa na marais wawili, Rais  Dk Samia Suluhu Hassan na Rais Dk Hussein  Ali Mwinyi. 

Pia  wanachama wa chama hicho wamekumbushwa wajibu  wa kuhubiri  maendeleo  yaliofanyika kwa  muda mfupi  chini ya maraisi hao wawili.

Ushauri  huo umetolewa na Katibu wa Kamati  Maalum  ya NEC  Zanzibar, Idara ya Itikadi  ,Uenezi na Mafunzo, Khamis  Mbeto  Khamis , alipokuwa akizumgumza na wanachama wa  Taaisis inayojihusisha na Utetezi kwa  Mama katika Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui .

Mbeto  alisema  majukumu ya kumtetea Mama , Rais Dk Samia yaendelee , yafanyike kwa kasi ya kutosha , usahihi na ufasaha, kwa kuonyesha  vielelezo, data na takwimu kwa kazi zilizotekelezwa na serikali zao tokea waliposhika madaraka. 

Alisema vipimo  vya utendaji na  utekelezaji wa sera ,ilani ya uchaguzi ya CCM ,miradi  ya maendeleo katika sekta zote, Rais Dk Samia na mwenzake Rais Dk  Mwinyi wametia fora.

" Timizeni wajibu wenu mkiwa Wakereketwa , makada wa chama, viongozi na  wanachama wa CCM. Nyinyi wana CCM mkinyamaza wapinzani watapotosha.Njia pekee bora ni  kusimama na kuelezea yote yaliofanyika"Alisema Mbeto. 

Aidha Katibu huyo  Mwenezi, aliishauri Taasisi hiyo  kutofanya kazi hiyo  kwa kupiga  maneno  matupu,  badala yake ikusanye data, takwimu na vielelezo vitakavyoonyesha  utendaji  kazi kwa vitendo. 

"Binadamu  tuna kawaida na hulka ya kuona vitu  na kusahau haraka. Hivyo  ni wajibu wenu  kuendelea kutangaza kazi zilizotekelezwa kisekta. Fanyeni kazi hii bila kuchoka kwakuwa siasa ni kazi ya kujitolea kufa na kupona "Alieleza.

Alisema marais   Dk Samia  na mwenzake  Rais Dk Mwinyi  uongozi wao, utaacha alama nyingi za kimaendeleo  ambazo hazitafutika na kusahaulika miaka kwa miaka . 

"Hata wapinzani wetu wakiwa peke yao wanakiri kazi kubwa imefanyika. Tanzania na Zanzibar  ya jana na juzi sio ya leo. Hawataki kutamka hivyo hadharani wakiamini vyama vyao vitakufa" Alisiaitiza Mbeto 

Kadhalika  aliongeza kusema maendeleo yanaonekana waziwazi katika  sekta zote muhimu za   Afya, Elimu, Ujenzi wa Miundombinu , Maji , Kilimo,  Ufugaji ,Uvuvi, Nishati ,Utalii na uwekezaji .

0/Post a Comment/Comments