Na Ester Maile Dodoma
Serikali kupitia wizara ya mifugo na Uvuvi imejipanga kuanza kuchumba visima vya maji karibu na majosho ili kuweza kurahisisha upatikanaji wa maji wakati wa kutibu mifugo .
Ameyaeleza hayo Waziri wa mifugo na uvuvi Dkt Ashatu Kachwamba Kijaji wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari leo jijini Dodoma katika kueleza mafanikio katika sekta ya mifugo na uvuvi kwa kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan.
Kijaji amewataka wafugaji kutenga maeneo ya marisho ilikuepusha migogoro kati ya wakulima na wafugaji pia kuacha kufuga kimazowea.
Hata hivyo wizara ya mifugo na uvuvi imejipanga kutoa chanjo kwa mifugo ili kuikinga mifugo na magonjwa mbalimbali ambapo asilimia sabini ya mifugo zinatakiwa kuchanjwa .
Vile vile amewataka wafugaji kufuga kisasa ili kuendana na soko linavyotaka kwani tumekuwa tukifuga mbuzi wenye vichwa vikubwa na siyo Ngo'mbe tunavyofikiria "Ameyasema Ashatu"
Post a Comment