IRENE LUOGA MFANYAKAZI HODARI TCDC MWAKA 2025/2026

********
Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC) imemtangaza Irene Luoga, Afisa Ushirika Mwandamizi kutoka Ofisi ya Mrajis Msaidizi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Mbeya, kuwa mfanyakazi hodari kwa mwaka 2025/2026.

Tuzo hiyo imetolewa kufuatia mchango wake mkubwa katika kusimamia na kuendeleza shughuli za ushirika, ikiwa ni pamoja na kuhamasisha uwajibikaji, uwazi na ufanisi katika Sekta ya ushirika.

Katika kipindi hicho, Irene ameonyesha weledi wa hali ya juu katika utekelezaji wa majukumu yake, akisimamia vyema shughuli mbalimbali za maendeleo ya Ushirika na kutoa msaada wa kitaalamu kwa wanachama na viongozi wa vyama. Juhudi zake zimechangia kuimarika kwa utendaji wa vyama vingi pamoja na kuongeza imani ya wanachama katika sekta ya ushirika nchini.

Akizungumza mara baada ya kupokea tuzo hiyo, Irene alieleza shukrani zake kwa Uongozi wa TCDC kwa kutambua mchango wake, akiahidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii zaidi.

 “Ninawashukuru sana TCDC kwa kunichagua kuwa mfanyakazi hodari wa mwaka huu.Hii ni heshima kubwa kwangu na inanipa motisha ya kuendelea kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na ufanisi zaidi ili kuleta maendeleo chanya katika sekta ya ushirika nchini na Taifa kwa ujumla,” alisema Irene.

 

0/Post a Comment/Comments