WATANZANIA WATAKIWA KUTOMUHUSISHA NDEGE AINA YA BUNDI NA IMANI ZA KISHIRIKINA.


ndege aina ya Bundi

NA ISSA MOHAMED

Watanzania wametakiwa kuacha imani potofu kuhusu ndege aina ya Bundi ambayo amekuwa akihusishwa na imani za kishirikina huku tafiti za kisayansi zikionesha ndege huyo hausiani kabisa na imani hizo.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mapema leo jijini Dar es salaam Mkuregenzi Mtendaji wa taasisi ya Mafia Ornithological and research centre Mackubi Joseph amesema Ndege huyo ana huwezo wa kunusa chembe hai ikiwa  mgonjwa anakaribia kufa hivyo hutumia kama chakula.

Amesema bundi ana uwezo wa kunusa harufu ya chembe hai zinazokaribia kufa ambapo harufu hiyo humsukuma kufika katika eneo hilo ambapo wazee wa zamani walimtumia ndege hiyo kama ishara mbaya endapo nyumba hiyo kuna mgonjwa.

Sambamba na hilo Mackubi amesema kufuatia mabadiliko ya Tabianchi pamoja na shughuli za binadam imepeleka zaidi ya makundi hamsini ya ndege wapo hatarini kupokea nchini ikiwa hatua za makusudi hazijachukuliwa ndege hao ni pamoja na Vocha.

Baadhi ya wakazi katika kijiji cha simbaulanga wilayani Kibiti mkoani Pwani wamesema kwa miaka mingi ndege wametumika kama viashiria vya kijadi ila kwa sasa ndege hao hawaonekani kwa kiasi kikubwa.

Kwa mujibu wa ripoti ya umoja wa mataifa –UN ya mwaka 2020 imeonesha upotevu wa bioanuwai umefikia rekodi ya viwango vya juu ambapo hekta bilioni mbili za ardhi zimepoteza rutuba yake huku zaidi ya aina milioni moja za wanyama na mimea katika sayari dunia viko katika hatari ya kutoweka.

1/Post a Comment/Comments

  1. Kweli tumekua tukiamini hivy onakufundishwa hivyo na wazeewetu tubadidilshe mtazamo hasi tuchukue hatua

    ReplyDelete

Post a Comment