COSOTA YASAJILI KAZI ZAIDI YA 500 ZA WASANII.



***********

 Chama cha hakimili Tanzania (COSOTA),kimesema kimesajili kazi za wasanii Zaidi ya 500,na wajivunia utendaji wao kazi kupitia mifumo waliojiwekea.

Hayo yamebainishwa leo mapema Jijini Dar es Salaam na Afisa uhusiano wa Cosota  Anita Jonas wakati akizungumza na waandishi habari kwenye maonyesho ya 48 ya Biashara Nchini maarufu Saba Saba .

Anita amesema wao kama Cosota wanajivunia kuwakutanisha wadau wao husususani wa kazi za Ubunifu na hakimili, pamoja na kuhamasisha wadau wengine kwenda kwenye Banda lao kusajili kazi na Ubunifu ili kuepusha wizi na udurufu WA kazi zao

 Hata hivyo,Anita amesema Sanaa na Ubunifu ni kazi kama zilivyo kazi zingine hivyo zinapaswa kulindwa na kuheshimika lakini pia kumnufanisha muhusika ambaye ametumia jasho lake katika Ubunifu WA kazi zake.

 Vilevile Anita ametoa wito kwa jamii Nchini kuhakikisha wanabadili mtazamo wao kuwa Sanaa ni kazi Rasmi, badala yake wanitumie kazi ya sanaa kama fursa za kujipatia ajira ya kipato kwa ngazi ya familia au mtu mmoja mmoja na hatimaye Taifa kwa ujumla.

 Katika hatua nyingine Anita ametoa wito kwa wadau husususani wale wanatoa mirabaha kwa wasanii waangalie thamani ya kazi za wasanii ili kuweza kumnufanisha msanii aliyebuni na kufanikisha Kazi husika kwani kwa kufanya hivyo kutaleta tija kwa msanii husika.

 Vilevile,Anita amemshukuru,  Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea Kuthamini na kuheshimu mchango mkubwa WA kazi za wanasanii na wabunifu hivyo amewaomba wadau wengine kuunga mkono juhudi hizo katika kuleta maendeleo ya Taifa kupitia kazi za Sanaa na Ubunifu,pia kuwahimiza wasanii kwenda kusajili kazi zao Cosota ili kuepusha usumbufu WA wizi au udurufu WA kazi zao.

 



 


 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

0/Post a Comment/Comments